Pata taarifa kuu

Washington iko tayari kubadilisha mkakati wa kufikia upunguzaji wa silaha za nyuklia

Marekani inaelekea kwenye mtazamo mpya kuhusu suala la Korea Kaskazini. Kwa vyovyote vile, hivi ndivyo maafisa wa kidiplomasia wa Marekani wamekuwa wakiwasilisha tangu mwanzoni mwa wiki hii. Kutokana na kushindwa kwa majadiliano ya kuachana na mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini na kuzuka upya kwa mvutano kwenye rasi hiyo, Washington inapanga mbinu mpya ya mazungumzo na utawala wa Kim Jong-un.

Mtu huyu anatazama ripoti ya televisheni inayoonyesha kipindi cha habari chenye picha za kumbukumbu za jaribio la kombora la Korea Kaskazini, katika kituo cha treni mjini Seoul mnamo Oktoba 19, 2021.
Mtu huyu anatazama ripoti ya televisheni inayoonyesha kipindi cha habari chenye picha za kumbukumbu za jaribio la kombora la Korea Kaskazini, katika kituo cha treni mjini Seoul mnamo Oktoba 19, 2021. AFP - ANTHONY WALLACE
Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu wa Seoul, Célio Fioretti

Kwa upane wa Marekani, kutokomeza silaha za nyuklia kwa utawala wa Korea Kaskazini bado ndio lengo. Lakini mtazamo wa Marekani kwa swali la Korea Kaskazini umebadilika ghafla, kama alivyotangaza Mira Rapp-Hopper, mshauri wa Joe Biden katika ukanda wa Asia:

"Katika swali la jinsi tunavyofikiria juu ya malengo yetu, Marekani inaendelea kujitolea kwa kutokomeza silaha za nyuklia katika rasi ya Korea. Lakini tuko tayari kuzingatia hatua za kati kuelekea uondoaji wa nyuklia. Hatua hizi zitafanya ukanda mzima na dunia kuwa salama. Tuko tayari kujadiliana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Korea ili kupunguza vitisho, haswa kwa kuzingatia hali ya sasa. "

Nyuma ya wazo la "hatua za kati" kuna kuachwa kwa sera ya kupokonya silaha mara moja. Kuanzia sasa, Washington ingependelea kutoa makubaliano kwa Kim Jong-un badala ya kusitishwa kwa muda kwa mpango wa nyuklia, kama ishara ya nia njema. Sera hii ya hatua kwa hatua lazima, hata hivyo, iongoze katika kukomeshwa kwa silaha za serikali.

Mabadiliko ya mtazamo ambayo yanaitia wasiwasi Seoul. Hakika, mbinu hii ya utawala wa Biden ndiyo iliyopendelewa na Donald Trump. Donald Trump amesifu Marekani ambayo ni salama dhidi ya Korea Kaskazini. Wakati kinyang'anyiro cha kuwania Ikulu ya Marekani bado hakina uhakika, Korea Kusini inahofia kupatana na rais huyo wa zamani wa Marekani, jambo ambalo wengine wanalichukulia kama kukiri udhaifu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.