Pata taarifa kuu

Qatar kushiriki katika uchimbaji wa gesi katika pwani ya Lebanon

Uchimbaji wa gesi kusini mwa Lebanon hatimaye utaanza hivi karibuni. Qatar iliingia, mnamo Jumapili Januari 29, kama TotalEnergies ya Ufaransa na ENI ya Italia katika muungano wenye dhamana ya kuendesha shughuli zake za uchimbaji gesi katika eneo hili la bahari kwenye mpaka na Israel.

Waziri wa Masuala ya Nishati na Mwenyekiti na Mkurugenzi Mkuu wa QatarEnergy Saad Sherida al-Kaabi (kushoto), akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya kimataifa ya mafuta na gesi ya Italia ENI Claudio Descalzi, Kaimu Waziri wa Nishati wa Lebanon Walid Fayad na Mkurugenzi Mkuu wa Total Energies Patrick Pouyanne , wakati wa hafla ya kutia saini kwa pamoja uchunguzi wa gesi baharini katika mji mkuu wa Beirut, Januari 29, 2023.
Waziri wa Masuala ya Nishati na Mwenyekiti na Mkurugenzi Mkuu wa QatarEnergy Saad Sherida al-Kaabi (kushoto), akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya kimataifa ya mafuta na gesi ya Italia ENI Claudio Descalzi, Kaimu Waziri wa Nishati wa Lebanon Walid Fayad na Mkurugenzi Mkuu wa Total Energies Patrick Pouyanne , wakati wa hafla ya kutia saini kwa pamoja uchunguzi wa gesi baharini katika mji mkuu wa Beirut, Januari 29, 2023. AFP - ANWAR AMRO
Matangazo ya kibiashara

Qatar itashikilia 30% ya hisa katika muungano huu, dhidi ya 35% kwa TotalEnergies na 35% kwa ENI. Emirate ya Ghuba inachukua nafasi ya Novatek ya Urusi, ambayo ilijiondoa katika mradi huo mnamo 2022.

Ushiriki wa Qatar sio tu kwamba unatoa msaada wa kifedha kwa mradi huu, lakini zaidi ya yote unajumuisha dhamana ya kisiasa, hasa kwa sababu ya uhusiano uliopo kati ya Qatar na nchi za Magharibi na hata Israel, amebaini mtaalamu wa nishati Naji Abi Aad akihojiwa na shirika la habari la AFP.

Kwa hivyo uchunguzi unaweza kuanza katika uwanja unaowezekana wa Kana, ambao sehemu yake iko katika maji ya eneo la Israeli. Israel itapokea fidia ya kifedha kulingana na makubaliano yaliyotiwa saini mwaka jana na Lebanon baada ya upatanishi wa muda mrefu wa Marekani.

Kulingana na Mkurugenzi Mkuu wa TotalEnergies, mchakato wa uchimbaji unapaswa kukamilika kwa takriban mwaka mmoja. Ugunduzi unaowezekana wa gesi utakuwa pumzi ya matumaini kwa Lebanon iliyotumbukia katika mzozo wa kiuchumi ambao haujawahi kutokea. Lakini nchi hii italazimika kusubiri miaka kadhaa kabla ya uzinduzi wa uzalishaji.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.