Pata taarifa kuu
USALAMA WA RAIA

Watu 19 wafariki baada ya barabara kuu kuporomoka kusini mwa China

Takriban watu 19 wamefariki baada ya barabara kuu kuporomoka katika jimbo la Guangdong kusini mwa China leo Jumatano, vyombo vya habari vya serikali vimesema.

Picha hii ya angani iliyopigwa tarehe 22 Aprili 2024 inaonyesha mtazamo wa jumla wa majengo na mitaa iliyofurika baada ya mvua kubwa kunyesha katika mji wa Qingyuan, mkoani Guangdong kusini mwa China.
Picha hii ya angani iliyopigwa tarehe 22 Aprili 2024 inaonyesha mtazamo wa jumla wa majengo na mitaa iliyofurika baada ya mvua kubwa kunyesha katika mji wa Qingyuan, mkoani Guangdong kusini mwa China. AFP - STR
Matangazo ya kibiashara

Magari 18 "yalinaswa" kutokana na kuporomoka kwa barabara kuu hiyo, shirika la utangazaji la CCTV limesema, tukio hilo "limehusisha watu 49, 19 kati yao walithibitishwa kufariki."

Maisha ya waliolazwa hospitalini hayako hatarini, CCTV imesema.

Picha zilizorushwa kwenye mitandao ya kijamii na kuripotiwa katika vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha moshi na miali ya moto ikipanda kutoka kwenye shimo refu ambapo magari hayo yalitumbukia. Mamlaka imetangaza kutumwa kwa karibu watu 500 kusaidia juhudi za misaada, kulingana na vyombo vya habari vya serikali.

Sababu ya kuporomoka kwa barabara kuu hiyo bado haijatajwa.

Mkoa wa Guangdong umekumbwa na mfululizo wa matukio mabaya ya hali ya hewa katika wiki za hivi karibuni, kuanzia mafuriko mabaya hadi kimbunga kiharibifu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.