Pata taarifa kuu
USALAMA-SIASA

Slovakia: Waziri Mkuu Robert Fico ajeruhiwa kwa risasi

Waziri Mkuu wa Slovakia Robert Fico amejeruhiwa kwa risasi leo Jumatano  baada ya kutoka kwenye mkutano wa serikali, shirika la habari la TASR linaripoti, likimnukuu Naibu spika wa Bunge, Lubos Blaha. Kulingana na vyombo vya habari vya ndani, amelazwa hospitalini. Mshukiwa ameripotiwa kukamatwa.

Vyombo vya usalama vinamuingiza Robert Fico ndani ya gari lake baada ya kujeruhiwa kwa risasi mnamo Mei 15, 2024 huko Handlova.
Vyombo vya usalama vinamuingiza Robert Fico ndani ya gari lake baada ya kujeruhiwa kwa risasi mnamo Mei 15, 2024 huko Handlova. REUTERS - Radovan Stoklasa
Matangazo ya kibiashara

Kulingana na kituo cha habari cha Slovakia TA3, mshambuliaji alimpiga risasi nne kiongozi huyo anayeunga mkono Urusi  na risasi moja tumboni. Mwandishi wa habari wa REUTERS katika eneo la tukio, nje ya mji mkuu Bratislava, alisikia milio kadhaa ya risasi na kuona polisi wakimkamata mshukiwa. Sababu ya shambulio hilo bado haijajulikana.

Rais wa Slovakia Zuzana Caputova amelaani shambulio la "kinyama" na kumtakia ahueni njema Robert Fico, ambaye alikua Waziri Mkuu tena mwaka jana baada ya kuwa tayari kushika wadhifa huu kati ya mwaka 2012 na 2018. Kiongozi huyo alijipambanua haswa kwa kukataa kuendelea kusaidia Ukraine kijeshi dhidi ya uvamizi wa Urusi.

(Taarifa zaidi zinakujia...)

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.