DRC: Watu zaidi ya 5 wauawa katika shambulio la mabomu Kimachine
Watu wanaoshukiwa kuwa waasi wa kundi la M23, kutoka ngome zao za juu katika eneo la Masisi, wamerusha mabomu katika kambi ya watu waliotoroka makaazi yao huko Kimachine, kwenye barabara ya Goma-Sake.
Imechapishwa:
KIMASHINE
#RDC : Comme devenu coutume, l’armée rwandaise #RDF et ses supplétifs terroristes du #M23 dans leur barbarie habituelle ont une nouvelle fois attaqué un camp des déplacés.
— Patrick Muyaya (@PatrickMuyaya) May 3, 2024
Au camp des déplacés de #Mugunga ce matin, l’horreur dans sa forme la plus grave !
Une bombe sur des… https://t.co/AutKOrtQft
Hayo yanajiri wakati waasi wa M23, wakiungwa mkono na jeshi la Rwanda kulingana na vyanzo mbalimbali vikinukuliwa na Radio OKAPI, wamedhibiti mji wa madini wa Rubaya, eneo la Masisi katika mkoa wa Kivu Kaskazini, tangu Jumanne Aprili 30.
Mkuu wa idara ya madini katika mkoa wa Kivu Kaskazini, Yvette Mwanza, anathibitisha kuwa kutokana na uvamizi wa mgodi huu, mapato makubwa hayataingia katika hazina ya serikali.
Kulingana afisa huyo, mgodi wa Rubaya ndio kitovu cha uchumi wa sekta ya madini huko Kivu Kaskazini katika suala la mapato ya mkoa:
"Uzalishaji wa Coltan katika Rubaya pekee unawakilisha 50% ya uzalishaji wa kitaifa."