Tuzo ya Marc-Vivien Foé mwaka wa 2024
Tuzo ya RFI-FRANCE 24 kumuenzi aliyekuwa mchezaji wa Marc-Vivien Foé, aliyewahi kuichezea klabu ya Lyon, raia wa Cameroon kabla ya kifo chake uwanjani mwaka 2003.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Tuzo hii imekuwa ikitolewa kila mwaka tangu mwaka 2009, kwa mchezaji kutoka barani Afrika, aliyefanya vizuri kwenye ligi ya soka nchini Ufaransa.
Mshindi wa msimu wa mwaka 2023/24 atafahamika tarehe 13 mwezi huu.
Wachezaji watatu wanaowania tuzo hiyo ni pamoja :
Pierre-Emerick Aubameyang, Mshambuliaji (Gabon/Marseille)
Aliwahi kushinda tuzo hili mwaka wa 2013 wakati akiichezea klabu ya AS Saint-Étienne na amekuwa na msimu bora tangu kujiunga na Marseille kama mchezaji huru.
Kwa sasa ana magoli 22 katika mashindano yote.
Nabil Bentaleb - LOSC Lille/Algeria
Licha ya timu yake ya taifa kuondolewa mapema katika mashindano ya AFCON mwaka huu, ameonyesha mchezo bora na klabu yake licha ya kukabiliwa na jeraha, mchezo wake umeonekana kumvutia kocha wake Paulo Fonseca.
Achraf Hakimi - Paris Saint-Germain/Morocco
Hakimi licha ya kuonyesha mchezo bora na timu yake ya taifa katika mechi za Afcon, amekuwa nguzo muhimu kwa kikosi cha kocha Luis Enrique.
Soma piaDRC: Chancel Mbemba ndiye mshindi wa tuzo za Marc-Vivien Foé 2023
Tuzo ya msimu uliopita, ilimwendea Chancel Mbemba, kutoka klabu ya Marseille, raia wa DRC.