Pata taarifa kuu

Nigeria: Alex Iwobi akabiliwa na vitendo vya uonevu mtandaoni

Nairobi – Nahodha wa timu ya taifa ya kandanda ya Nigeria Super Eagles amekuwa wa hivi punde kutoa  wito wa kukomeshwa kwa vitendo vya uonevu mtandaoni dhidi ya kiungo Alex Iwobi.

Alex Iwobi amekabiliwa na mashambulio kwenye mitandao ya kijamii baada ya Nigeria kushindwa kwenye fainali ya AFCON
Alex Iwobi amekabiliwa na mashambulio kwenye mitandao ya kijamii baada ya Nigeria kushindwa kwenye fainali ya AFCON REUTERS - SIPHIWE SIBEKO
Matangazo ya kibiashara

Mashabiki kadhaa wa soka wa Nigeria wamemtusi Iwobi kwenye mitandao ya kijamii, wakimlaumu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 baada ya nchi yao kufungwa 1-2 na Ivory Coast katika mchezo wa fainali ya Afcon siku ya Jumapili.

Iwobi alicheza kwenye mechi hiyo kwa dakika 79, kabla ya kundolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Alhassan Yusuf.

Nigeria ilishindwa kwenye fainali ya Afcon na Ivory Coast
Nigeria ilishindwa kwenye fainali ya Afcon na Ivory Coast © Pierre René-Worms/RFI

Iwobi amelazimika kufuta picha zake za Instagram siku ya Jumatatu baada ya kukabiliwa na uonevu huo kwenye mitandao ya kijamii.

Nahodha wa Super Eagles Ahmed Musa na baadhi ya raia  wengine wa Nigeria  wamemtetea Iwobi, wakilaani mashambulizi yaliyolengwa mtandaoni dhidi ya mchezaji huyo na kusema si haki kumtenga baada ya timu yao kupoteza.

Wachezaji wa timu ya taifa ya Nigeria wakati wa mechi yao dhidi ya Ivory Coast kuwania ubingwa wa Afcon
Wachezaji wa timu ya taifa ya Nigeria wakati wa mechi yao dhidi ya Ivory Coast kuwania ubingwa wa Afcon REUTERS - LUC GNAGO

Iwobi bado hajazungumza lolote kuhusu mashambulizi dhidi yake kwenye mitandao ya kijamii.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.