Pata taarifa kuu
UKRAINE

Uwanja wa ndege wa Crimea nchini Ukraine waendelea na shughuli zake licha ya taarifa za kutekwa na watu wenye silaha

Uwanja wa mjini Crimea nchini Ukraine umeripotiwa kuendelea na shughuli zake za kawaida hii leo licha ya kuwepo kwa taarifa kuwa uwanja huo ulikuwa umetekwa na watu wenye silaha.

Polisi wakiwa kwenye Uwanja wa ndege wa Crimea nchini Ukraine kuhakikisha usalama
Polisi wakiwa kwenye Uwanja wa ndege wa Crimea nchini Ukraine kuhakikisha usalama www.startribune.com
Matangazo ya kibiashara

Taarifa zinaeleza kuwa abiria wanaendelea kuingia katika uwanja huo wa ndege kama kawaida kwa ajili ya safari zao.

Hayo yanakuja wakati huu mataifa yenye nguvu yakionya kuhusu hatua ya kuingilia masuala ya Ukraine ambayo inakabiliwa na hali ya sintofahamu baada ya rais Victor Yanukovich kuondolewa madarakani.

Waziri wa ulinzi wa Marekani Chuck Hagel ametoa angalisho kwa mataifa kutoingilia mipaka ya Ukraine.

Kwa upande wake waziri mkuu wa Uingereza David Cameron amesema kuwa nchi ya Urusi inapaswa itekeleze ahadi yake ya kutoingilia mipaka ya Ukraine.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.