Pata taarifa kuu

DR Congo yasonga mbele michuano ya AFCON, Tanzania yafungishwa virago

Timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, imefuzu katika hatua ya 16 bora, kuwania kombe la mataifa ya Afrika, baada ya kutofungana na Tanzania kwenye mechi ya mwisho ya hatua makundi, Jumatano usiku.

Mchezaji wa DRC Yoane Wissa akimenyana na Watanzania Novatus Miroshi na  Bakari Nondo kwenye mchuano wa  mwisho wa kundi F mjini Korhogo, Januari 24, 2024.
Mchezaji wa DRC Yoane Wissa akimenyana na Watanzania Novatus Miroshi na Bakari Nondo kwenye mchuano wa mwisho wa kundi F mjini Korhogo, Januari 24, 2024. © AP / Themba Hadebe
Matangazo ya kibiashara

Matokeo hayo, yameiondoa Tanzania kwenye michuano hiyo baada ya kumaliza kundi la F kwa alama 2. Taifa Stars ilianza vibaya baada ya kufungwa na Morocco mabao 3-0 na ikatoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Zambia.

Mara tatu ambayo imecheza michuano hii mikubwa barani Afrika 1980, 2019 na 2023 haijawahi kushinda mechi yoyote.

Ushindi wa Morocco wa bao 1-0 dhidi ya Zambia, iliisaidia wenyeji Cote Dvoire kusonga mbele kama mojawapo ya timu iliyomaliza katika nafasi ya tatu bora katika kundi la A.

Wachezaji wa timu ya taifa ya Morocco wakishangalia ushindi kwenye mechi mojawapo ya AFRON 2023
Wachezaji wa timu ya taifa ya Morocco wakishangalia ushindi kwenye mechi mojawapo ya AFRON 2023 © AFP / SIA KAMBOU

Katika hatua nyingine, kocha wa Tunisia Jalel Kadri, ametangaza kujiuzulu baada ya timu yake kuondolewa kwenye michuano hiyo.

“Naondoka kwa sababu mkataba wangu ulinitaka nifike kwenye hatua ya nusu fainali, kwa sababu hatujafikia hapo, mkataba wangu umekwisha,” amesema.

Tunisia imeondoka kwenye michuano hiyo, bila ya kushinda hata mechi moja katika kundi E.

Ameugana na makocha wa wenyeji Cote Dvoire, Ghana na Algeria ambao wameachishwa kazi wiki hii kwa sababu ya matokeo mabaya.

Ratiba ya hatua ya 16 bora

Jumamosi  27/01/2024

  • Angola  vs  Namibia
  • Nigeria  vs  Cameroon

Jumapili  28/01/2024

  • Equatorial Guinea vs  Guinea
  • Misri  vs Congo DR

Jumatatu  29/01/2024

  • Cabo Verde vs  Mauritania
  • Senegal vs  Côte d'Ivoire

Jumanne  30/01/2024

  • Mali vs Burkina Faso
  • Morocco vs Afrika Kusini

     

     

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.