Pata taarifa kuu
OM-SOKA

Soka-OM: Abou Diaby kushiriki mchuano dhidi ya Gérone

Abou Diaby hatimaye atakua katika kikosi cha wachezaji kumi na moja cha OM ambacho kinachuana Jumatano hii usiku dhidi ya Gérone mechi yao ya kirafiki. OM watakua ugenini.

Abou Diaby (katikati, akivaa jezi za blu) dhidi ya Finland.
Abou Diaby (katikati, akivaa jezi za blu) dhidi ya Finland. REUTERS/Antti Aimo-Koivisto/Lehtikuva
Matangazo ya kibiashara

Abou Diaby, ambaye hajacheza mchezo wa maandalizi kutokana na jeraha la kifundo cha mguu wake wa kushoto alilolipata mwishoni mwa msimu uliopita, atakuwa miongoni mwa wachezaji kumi na mmoja watakao anza mechi hii.

Kocha wa OM Franck Passi, anasema ana imani kwamba Abou Diaby ataonyesha umaarufu wake, baada ya kupona jeraha alilokua akiuguza

Kikosi cha OM kinaundwa na Pelé, Sakai, Hubocan, Doria, Bedimo, Diaby, Machach, Alessandrini (katikati), Cabella, Khaoui, Gomis

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.