Timu ya wanawake ya mpira wa miguu ya ufaransa yaingia nusu fainali michuano ya Olympiki
Timu ya taifa ya wanawake ya mpira wa miguu ya Ufaransa imefaanikiwa kuingia nusu fainali katika michuano ya olmpiki inayoendelea jijini London nchini Uingereza baada ya kuitandika Sweden mabao 2-1
Imechapishwa:
Katika mchezo huo, wachezaji wa Ufaransa walionyesha mchezo mzuri na kuhimili mikiki ya wachezaji wa Sweden ambao waliendesha mashambulizi mara kadhaa kuhitaji ushindi bila mafaanikio.
Ufaransa itacheza nusu fainali kati ya Brazil au Japan. Licha ya kuingia katika nusu fainali, kina dada hao wa timu ya taifa ya Ufaransa waliendesha juhudi za ziadas katika kufikia hatuwa hiyo, kwani walipata mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa wapinzani wao wa Sweden.