Michuano ya Olympiki yaingia katika siku yake ya saba
Michuano ya Olympiki imeingia katika siku yake ya saba leo alhamisi, wakati nchi ya China ikiongoza kwa kubeba medali nyingi za dhahabu na fedha, ikifuatiwa na Marekano. hadi sasa China inaongoza kwa medali 17 za dhahabu.
Imechapishwa:
China ndio ambayo inawakilisha vema katika michuano hiyo baada ya wachezaji wake kujinyakulia medali nyingi katika michuano mbalimbali. hadi sasa China imekwisha nyakuwa medali 17 za dhahabu, 9 zaa fedha na 4 za shaba, ikiwa na jumla ya medali 30.
Marekani inachukuw anafasi ya pili ikiwa na medali 13 za dhahabu, 8 za fedha na 9 za shaba, ikiwa na jumla ya medali 30. China inashinda Marekani uwingi wa medali za dhahabu.
Corea Kusini inachukuwa nafasi ya tatu ikiwa na medali 6 za dhahabu ikifuatiwa na Ufaransa yenye medali 5 za dhahabu.
Upande wa Afrika, Afrika Kusini ndio ambayo inaongoza hadi sasa kwa medali 3 za dhahabu.