Pata taarifa kuu
Uingereza

FA kumtaja Mrithi wa Fabio Capello

Shirikisho la soka nchini Uingereza, limeanza Mchakato wa kuanza kumpata Kocha mpya wa timu ya Taifa ya Uingereza baada ya Fabio Capello kujiuzulu wadhifa huo kufuatia sakata la John Terry.

aliyekuwa Kocha wa Timu ya Taifa ya Uingereza, Fabio Capello.
aliyekuwa Kocha wa Timu ya Taifa ya Uingereza, Fabio Capello. REUTERS/Andrew Winning
Matangazo ya kibiashara

Kumekuwa na tetesi kuwa huenda Kocha wa tottenham hotspur, Harry Redknapp akamrithi Capello aliyejiuzulu usiku wa jana baada ya kuukosoa hadharani uamuzi FA kumvua unahodha Mchezaji wa Chelsea, John Terry.

Uamuzi wa Capello wa kushtukiza umefanyika wakati ambapo pia Kocha wa Tottenham kukutwa hana hatia na mahakama ya Southwark alipokuwa akikabiliwa na shutma za kukwepa kulipa Kodi.

FA itafanya mkutano na waandishi wa Habari hii leo ili kumteua mrithi kabla ya Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya, michuano itakayopigwa Miezi minne ijayo.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.