Pata taarifa kuu
club bingwa

Man United kucheza fainali na Barcelona

Timu zitakazokutana fainali ya klubu bingwa barani Ulaya sasa zimejulikana. Manchester United ya Uingereza itakutana na Barcelona ya Uispania.

Vijana wa Manchester United.
Vijana wa Manchester United. Reuters
Matangazo ya kibiashara

Manchester United itakutana na Barcelona kwenye fainali ya klabu Bingwa Ulaya baada ya kuicharaza Schalke 04 ya Ujerumani kwa magoli 4-1.

Magoli ya Manchester United yalifungwa na Antonio Valencia, Darron Gibson, na Anderson akufunga magoli mawili.
Katika mchezo wa kwanza Man United ilipata ushindi wa mabao 2-0.
Barcelona iliingia fainali baada ya kuifunga Real Madrid 3-1 baada ya michezo miwili ya nusu fainali.
Fainali ya Klabu Bingwa Ulaya itachezwa kwenye uwanja wa Wembley, tarehe 28 mwezi Mei.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.