Pata taarifa kuu

Kumi na moja wafariki na wengi hawajulikani waliko kufuatia maporomoko ya udongo Indonesia

Watu kumi na moja wamefariki na wengine 50 hawajilikani walipo Jumatatu, Machi 6, baada ya mvua kubwa kunyesha na maporomoko ya ardhi kuripotiwa kwenye Visiwa vya Riau, eneo lililo mbali na mji ni kati ya mbali zaidi katika visiwa vya Indonesia, imesema idara ya majanga ya asili,kulingana na shirika la habari la AFP.

Waathirika wa mafuriko huko Sentani, katika mkoa wa Papua, Indonesia, Machi 17, 2019.
Waathirika wa mafuriko huko Sentani, katika mkoa wa Papua, Indonesia, Machi 17, 2019. Antara Foto/Gusti Tanati/ via REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Mvua kubwa imesababisha maporomoko ya udongo nchini Indonesia. Angalau watu kumi na moja wameangamia na wengine 50 hawajulikani waliko, baada ya mvua kubwa na maporomoko ya udongo kwenye moja ya visiwa vya mbali zaidi katika visiwa vya Indonesia, shirika la kitaifa linalosimamia majanga ya asili lilmesema.

Janga hilo lilitokea kwenye Visiwa vya Riau, msemaji wa Shirika la majanga asilia, Abdul Muhari, mesema kwenye kituo cha runinga.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.