Pata taarifa kuu

Marekani yaionya Urusi kuwa itakabiliwa vikali ikitumia silaha za maangamizi dhidi ya Ukraine

Marekani kwa mara nyingine, imeionya Urusi kuwa itakabiliwa vikali, iwapo itatumia silaha za nyuklia kuishambulia Ukraine. 

Rais wa Urusi Vladimir Putin na Waziri wa Ulinzi wa Urusi Sergei Shoigu wakihudhuria ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa la Kijeshi na Kiufundi la 2022 katika Mbuga ya Patriot nje ya Moscow, Urusi, Jumatatu, Aug. 15, 2022.
Rais wa Urusi Vladimir Putin na Waziri wa Ulinzi wa Urusi Sergei Shoigu wakihudhuria ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa la Kijeshi na Kiufundi la 2022 katika Mbuga ya Patriot nje ya Moscow, Urusi, Jumatatu, Aug. 15, 2022. AP
Matangazo ya kibiashara

Wiki iliyopita, rais Vladimir Putin alionya kutumia kila mbinu ikiwemo silaha za nyuklia kuwalinda watu wake, huku akitangaza kuongeza idadi ya wanajeshi kwenda nchini Ukraine. 

Wakati huo huo, zoezi la kura ya maoni ya kutaka maeneo yanayodhibitiwa na wanajeshi wa Moscow  Mashariki na Kusini mwa Ukraine kuwa sehemu ya Urusi,  linaendelea. 

China na India zatoa wito kwa mazungumzo ya kumaliza vita nchini Ukraine

Watu katika eneo la Dagestan nchini Urusi wamekabiliana na polisi katika maandamano ya hivi punde kupinga hatua ya Urusi ya kusajili wanajeshi 300,000 wa akiba.

Zaidi ya watu 100 walikamatwa wakati wa maandamano katika mji mkuu wa mkoa wa Makhachkala, OVD-Info, mfuatiliaji huru wa haki za binadamu wa Urusi alisema.

Wakati huo huo China na India zimetoa mwito wa mazungumzo ya kumaliza vita vya Ukraine, na kuashiria kupungua kwa uungaji mkono thabiti katika sera ya uvamizi kwa mshirika wa jadi Urusi. 

Katika mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi amezitaka Urusi na Ukraine kuzuia mgogoro huo kuenea na kuathiri nchi zinazoendelea. Amesema suluhisho la msingi ni kushughulikia wasiwasi wa kiusalama wa pande zote na kuwa na muundo wa usalama wenye usawa, thabiti na endelevu. India kwa upande wake, ilisema kuwa inasimama katika msingi wa amani na kutoa wito wa mazungumzo na diplomasia kama suluhisho pekee. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.