NATO : Huenda nchi za Ulaya zikatatizika kupata gesi kutoka Urusi
Jumuiya ya majeshi ya kujihami ya nchi za Magharibi NATO, inahofia mataifa ya Ulaya yatatizika kupata gesi kutoka Urusi iwapo nchi hiyo itaivamia Ukraine.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Hali ya wasiwasi imeendelea kushuhudiwa katika mpaka wa Ukraine na Urusi, huku maelfu ya wanajeshi wa Moscow wakiendelea kufanya mazoezi.
Hata hivyo, Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg anasema suluhu inaweza kupatikana kabla ya uvamizi huo kufanyika.
Marekani ambayo imeonya kuwa huenda uvamizi huo ukafanyika mapema mwezi Februari, imeahidi kusimama na Ukraine, pamoja na mataifa ya Ulaya.