Pata taarifa kuu

Uingereza imesema idadi ya waomba hifadhi watakaotumwa Rwanda ni ndogo

Nairobi – Waziri wa mambo ya ndani wa Uingereaza, juma hili amesema kuwa huenda idadi ya wahamiaji watakaofukuzwa nchini humo chini ya makubaliano na nchi ya Rwanda, ikawa ndogo lakini itategemea na mambo mengine yatakayojitokeza.

Mpango wa kuwatuma wahamiaji nchini Rwanda kutoka Uingereza umekuwa ukipingwa mahakamani
Mpango wa kuwatuma wahamiaji nchini Rwanda kutoka Uingereza umekuwa ukipingwa mahakamani AFP - NIKLAS HALLE'N
Matangazo ya kibiashara

Waziri, James Cleverly, amewaambia wabunge kuwa makubaliano na taifa hilo la Afrika mashariki ni "sehemu moja tu" ya majibu ya serikali katika kukabiliana na uhamiaji haramu, akidai pia mikataba na nchi nyingine inaweza kuwa na "athari" kwa idadi itakayotumwa.

Hata hivyo, licha ya shinikizo kutoka kwa wabunge waliotaka kufahamu ni wahamiaji wangapi watapelekwa nchini Rwanda, waziri Cleverly, alikataa kutabiri ni watu wangapi wangefukuzwa na kwamba bado hawajukubaliana na Kigali kuhusu idadi yao.

Mpango wa Serikali umekuwa ukipingwa vikali na mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu
Mpango wa Serikali umekuwa ukipingwa vikali na mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu © Reuters

Kauli yake anaitoa wakati huu maswali kuhusu gharama ya mpango huo yakiongezeka baada ya kuibuka mwezi uliopita kuwa Uingereza imelipa pauni milioni 240 kwa Rwanda, licha ya mizozo ya kisheria, ikimaanisha kuwa bado hakuna mtu aliyepelekwa Rwanda.

Sheria ya kufufua mpango huo baada ya kuamuliwa kuwa ni kinyume cha sheria na mahakama ya juu ilipitishwa na wabunge mapema mwezi huu, lakini inatarajiwa kupata upinzani mkubwa katika bunge la wananchi.

Uingereza inalenga kupunguza idadi ya waomba hifadhi wanaowasili nchini humo kwa wingi wakitokea kaskazini mwa Ufaransa kwa kutumia boti ndogo.
Uingereza inalenga kupunguza idadi ya waomba hifadhi wanaowasili nchini humo kwa wingi wakitokea kaskazini mwa Ufaransa kwa kutumia boti ndogo. © Daniel Leal / AFP

Chini ya mpango huo wa miaka mitano, Uingereza itatuma idadi ambayo haijabainishwa ya wanaotafuta hifadhi nchini Rwanda - ambapo wanaweza kutuma maombi ya kuwa mkimbizi wakiwa huko au kutafuta hifadhi katika "nchi nyingine ya tatu ambayo ni salama".

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.