Pata taarifa kuu
AFRIKA KUSINI-CORONA-UCHUMI

Coronavirus: Afrika Kusini yajitaarisha kulegeza vizuizi zaidi

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amesema analenga kulegeza masharti zaidi ya watu kuendelea na shughuli zao za kawaida, wakati huu nchi hiyo inapoendelea kukabiliana na janga la Corona.

Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika ya Kusini amesema ana lengo la kuendelea kuondosha vizuizi zaidi vilivyowekwa katika kukabiliana na janga la virusi vya corona lakini katika maeneo ambayo yameathiriwa zaidi, vitaendelea kuwepo hadi Juni.
Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika ya Kusini amesema ana lengo la kuendelea kuondosha vizuizi zaidi vilivyowekwa katika kukabiliana na janga la virusi vya corona lakini katika maeneo ambayo yameathiriwa zaidi, vitaendelea kuwepo hadi Juni. REUTERS/Sumaya Hisham
Matangazo ya kibiashara

Hata hivyo, amesema maeneo ambayo kuna maambukizi zaidi, shughuli za kawaida zitaanza kurejea polepole mwezi Juni, huku akisisitiza kuwa lengo ni kuanza kurejesha nchi hiyo katika mfumo wake wa kawaida wa kiuchumi.

Afrika Kusini ina visa vya Corona zaidi ya Elfu 12, watu 4,745 wamepona na 219 wamefariki dunia kutokana na virusi hivyo.

Takribani watu 300,000 kote duniani wameripotiwa kufariki dunia kutokana na virusi vya Corona, na zaidi ya visa milioni 4.3 vimerekodiwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.