Vita nchini Ukraine: Urusi yauteka mji wa Kherson
Wanajeshi wa Urusi wanadai kuuteka mji wa Kherson, Kusini mwa Ukraine, wakati huu wanapoendeleza mashambulizi katika miji mbalimbali ya nchi hiyo na kusababisha maafa.
Imechapishwa:
Siku ya saba ya mashambulizi ya vikosi vya Urusi nchini Ukraine, mashambulizi yameendelea kushuhudiwa Katia miji ya Kaskazini, Mashariki na Kusini mwa nchi hiyo;
Licha ya wanajeshi wa Urusi kudai kudhibiti mji wa Kherson, uongozi wa mji huo unakanusha na badala yake unasema umezingirwa.
Tayari wanajeshi wa angaa w a Urusi wanaelezwa kuwasili katika mji wa Kharkiv, Kaskaini Mashiriki mwa nchi hiyo na mapigano makali yanaendelea kushuhudiuwa.
Ripoti zinasema, vikosi vya Urusi ambayo vinalenga mji mkuu Kyiv, vipo umbali wa Kilomita 25, Kaskazini mwa mji huo huku rais wa Ukraine Volodymry Zelenskyy akisema Urusi inalenga kuifuta nchi yake.