Pata taarifa kuu
UINGEREZA-COVID19

Uingereza yawa taifa la kwanza kuidhinisha chanjo ya Pfizer

Uingereza imekuwa nchi ya kwanza duniani kuidhinisha matumizi ya chanjo dhidi ya COVID-19 iliyotengenezwa na maabara ya Marekani ya Pfizer na mshirika wake BioNTech kutoka Ujerumani.

PICHA YA MAKTABA: Uingereza imekuwa taifa la kwanza duniani kuidhinisha chanjo ya Pfizer kutibu virusi vya Corona.
PICHA YA MAKTABA: Uingereza imekuwa taifa la kwanza duniani kuidhinisha chanjo ya Pfizer kutibu virusi vya Corona. REUTERS/Dado Ruvic/Illustration/File Photo
Matangazo ya kibiashara

"Chanjo hii itapatikana nchi nzima kuanzia wiki ijayo," serikali ya Uingereza imesema leo Jumatano katika taarifa.

 

Matumizi haya yameidhinishwa na mamlaka ya dawa nchini Uingereza, Medicines and Healthcare Products Regulatory Agency (MHRA), mamlaka ya afya ya kwanza duniani kuchukua uamuzi kama huo.

 

Hakuna chanjo yoyote ambayo imeidhinishwa katika nchi yoyote duniani.

 

"Hii ni habari njema sana," amesema Waziri wa Afya wa Uingereza Matt Hancock.

 

Katika taarifa, maabara ya Marekani ya Pfizer yamebaini kwamba dozi za kwanza zitaweza kutolewa "mara moja" na kusema kuwa idhini hii ya kwanza ni "mafanikio" katika vita dhidi ya janga COVID-19.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.