Bei ya vyakula kuongezeka mara mbili mwaka 2030 : OXFAM yaonya
Dunia huenda ikashuhudia upandaji maradufu wa bei ya vyakula vikuu katika kipindi cha miaka ishirini ijayo, iwapo viongozi wa ulimwengu hawatachukua hatua madhubuti, Shirika la Kutoa Misaada ya Chakula Oxfam limeonya.
Imechapishwa:
Oxfam imeanisha kuwa ifikapo mwaka 2030 huenda bei ya vyakula tegemezi duniani ikapanda kwa asilimia mia moja ishirini hadi mia moja na themanini, kitu ambacho kinaweza kuchangia wananchi kushindwa kumudu kujipatika mahitaji.
Kikubwa ambacho kinatajwa huenda kikachangia hali hiyo ni mabadiliko ya hali ya hewa pamoja na kupungua katika uwezekaji wa mazao ya vyakula ambao ulikuwa unafanywa hapo awali.
Chakula ni hitaji la muhimu kwa maisha ya binadamu, ambapo kama kinakosekana kinaweza kuhatarisha maisha ya mtu huyo, bila kujali ni umri, rangi wala ujinsia.