Pata taarifa kuu

Gaza: Israeli yadaiwa kuamuru kuondolewa kwa watu katika hosipitali ya Al-Shifa

Nairobi – Wanajeshi wa Israeli wamedaiwa kutaka watu walio katika hosipitali ya Al-Shifa kuondolewa kwa haraka, tangazo linalokuja wakati huu maofisa hao wa Israeli wakiendelea na oparasheni katika hosipitali hiyo kwa madai kuwa wapiganaji wa Hamas wanajificha humo.

Al-Shifa
Wahudumu wa afya katika hosipitali ya al-Shifa, wanasema agizo la Israeli ni ngumu kutekelezwa © Khader Al Zanoun / AFP
Matangazo ya kibiashara

Al-Shifa, ni hosipitali kubwa zaidi katika ukanda wa Gaza na imekuwa kitovu cha mapigano kati ya Israeli na wapiganaji wa Hamas wiki hii.

Agizo hilo linalodaiwa kutoka kwa jeshi la Israeli linakuja wakati huu makabiliano kati yake na wapiganaji wa Palestina, Hamas yakiingia wiki ya saba tangu Hamas kutekeleza shambulio tarehe 7 ya mwezi Oktoba Kusini mwa Israeli.

Wanajeshi wa Israeli wanasema Hamas wanatumia kituo hicho kama kituo chao chao cha kutoa kamandi
Wanajeshi wa Israeli wanasema Hamas wanatumia kituo hicho kama kituo chao chao cha kutoa kamandi via REUTERS - Israel Defense Forces

Israel imekuwa ikidadi kuwa wapiganaji wa Hamas wanatumia hosipitali ya Al-Shifa, kama kituo chao cha kamandi madai ya ambao Hamas imekanusha.

Umoja wa Mataifa umekadiria kuwa karibia wagonjwa 2,300, wahudumu wa hosipitali hiyo na raia wengine wa Palestina ambao walikuwa wanapewa hifadhi katika kituo hicho kabla ya uvamizi wa Israeli siku ya Jumatano.

Gaza, hôpital al-Chifa, les patients et réfugiés pêle-mêle dans les couloirs de l'hôpital, le 10 novembre 2023.
Hosipitali hiyo imekuwa ikitoa pia hifadhi kwa wakimbizi waliotoroka mapigano ya Hamas na Israeli AFP - -

Wizara ya afya katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa idadi kubwa ya wagonjwa waliofariki katika kituo hicho ilisababishwa na kukatwa kwa umeme, ukosefu wa mafuta uliosababishwa na mapigano mazito yanyoendelea.

Israel imekuwa ikisisitiza wagonjwa kuhamishiwa kusini mwa eneo hilo lakini wahudumu wa afya kwenye hosipitali hiyo wanasema kuwa wagonjwa hao hawawezi kuondolewa katika hali ya sasa.

Photo diffusée par l'armée israélienne le 15 novembre 2023 qui montre un soldat se tenant à l'extérieur de l'hôpital al-Chifa.
AI Shifa ndio hosipitali kubwa zaidi katika ukanda wa Gaza AFP - -

Kwa mujibu wa mkurungenzi mkuu katika hoispitali hiyo Mohammed Abu Salmiya amesema wanajeshi wa Israeli wamemtaka kuwaondoa wagonjwa, watu waliojeruhiwa na waliomba hifadhi pamoja na wahudumu wa afya na kuwapeleka katika eneo la kusini kwa miguu bila ya kutumia magari ya wagonjwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.