Pata taarifa kuu

Waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin anazuru Israeli

Waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin, amewasili nchini Israeli katika ziara inayolenga kuonyesha mshikamano na taifa hilo baada ya kushambuliwa na wapiganaji wa Hamas ambalo limesababisha vifo vya maelfu ya raia wake.

Hii ni ziara yake tatu nchini Israeli tangu kuteuliwa katika wadhifa huo
Hii ni ziara yake tatu nchini Israeli tangu kuteuliwa katika wadhifa huo REUTERS - KEVIN LAMARQUE
Matangazo ya kibiashara

Austin anatarajiwa kukutana na viongozi wa Israeli akiwemo waziri mkuu Benjamin Netanyahu, waziri wa ulinzi Yoav Gallant.

Hii ni ziara yake tatu nchini Israeli tangu kuteuliwa katika wadhifa huo na inakuja baada ya ile ya waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Antony Blinken katika eneo hilo.

Haya yanajiri wakati huu idadi ya waliouawa katika eneo la Gaza ikifikia 1,537 wakiwemo watoto kwa mujibu wa wizara ya afya ya Gaza.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani alikutana na waziri mkuu wa Israeli wakati akizuru nchi hiyo
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani alikutana na waziri mkuu wa Israeli wakati akizuru nchi hiyo via REUTERS - POOL

Kwa mujibu wa wizara hiyo, watu 500 waliouawa walikuwa chini ya umri wa miaka 18.

Tayari Israeli imewataka raia zaidi ya milioni moja wanaoishi katika eneo la kaskazini mwa Gaza kuondoka katika muda wa saa 24 kabla ya mashambulio ya ardhini yaliopangwa kuaanza, wito ambao wapiganaji wa Hamas wameukataa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.