Saudi Arabia: Tumefaulu kuvunja kundi la kigaidi
Saudi Arabia imetangaza kwamba imeangamiza kundi la kigaidi lililopewa mafunzo na kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi cha Iran, madai ambayo yamekanushwa na mamlaka nchini Iran.
Imechapishwa:
Mamlaka katika ufalme wa Kiwahabi, mpinzani mkubwa wa kikanda dhidi ya Iran, imebaini kwamba imewakamata magaidi kumi na silaha kadhaa pamoja na vilipuzi.
Washukiwa watatu waliokamatwa, walipewa mafunzo nchini Iran na wengine "wanashirikiana na kundi hilo ndogo la magaidi kwa shughuli tofauti, amesema msemaji wa ofisi ya rais wa usalama wa nchi.
Wanachama wa kundi hilo, ameongeza, "Magaidi hao walipewa mafunzo ya kijeshi, hasa kwa jinsi ya kutengeneza vilipuzi, katika maeneo ya vikosi vya Walinzi wa Mapinduzi nchini Iran" kwa wiki kadhaa mwishoni mwa mwaka 2017.