Baada ya mzozo wa majuma kadhaa nchini Misri hatimaye raia wa nchi hiyo wamepiga kura ya maoni kwa duru mbili na matokeo ya jumla yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi nchini humo yameipa ushindi kura ya ndiyo iliyokubali kupitishwa kwa rasimu hiyo. Kutazama mchakato huo pamoja na changamoto zilizojiri katika zoezi hilo tutakuwa na Profesa Mustapha Zakaria kutoka Mombasanchini Kenya na Jumanne Abdul kutoka Bujumbura nchini Burundi. Mtangazaji ni Ali Ali Bilal, karibu ujuike naye.