Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Rais wa Marekani Barack Obama afanikiwa kutetea wadhifa wake kwa kumuangusha Mitt Romney huku Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa UNSC likiongeza muda wa Majeshi ya AMISOM nchini Somalia
Imechapishwa:
Cheza - 20:08
Kura za majimbo mia tatu na tatu alizopigiwa Barack Obama dhidi ya mia mbili na sita za Mitt Romney zimesababisha Kiongozi huyo kushinda uchaguzi mkuu na kuendelea kuongoza kwa miaka minne zaidi, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa UNSC laongeza muda wa miezi minne kwa Majeshi ya Umoja wa Afrika Yanayolinda Amani nchini Somalia AMISOM na Wananchi wa Taifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC waendelea kushuhudia kuundwa kwa Makundi zaidi ya kisiasa na kuchochea ongezeko la wasiwasi wa usalama.