Rais wa Uganda Yoweri Museveni yuko nchini Kenya kwa ziara ya kikazi
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amewasili hapo jana jijini Nairobi nchini Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Imechapishwa:
Museveni anatarajiwa kushiriki mazungumzo na mwenyeji wake rais wa Kenya William Ruto hii leo alhamisi.
Rais Museveni alipokelewa na waziri wa mambo ya kigeni na mkuu wa mawaziri nchini Kenya, Musalia Mudavadi.
President Museveni is here for a three-day state visit, marking a significant step towards strengthening the fraternal bonds between our nations and fostering mutual prosperity and growth. pic.twitter.com/MowZ6y0K9a
— Musalia W Mudavadi (@MusaliaMudavadi) May 15, 2024
Ziara hiyo inafuatia kikao cha pili cha Tume ya Pamoja ya Mawaziri (JMC) kilichomalizika hivi karibuni kati ya Kenya na Uganda, ambapo mikataba saba ya makubaliano (MoU) ilisainiwa katika masuala mbalimbali ikiwemo utumishi wa umma, elimu, maendeleo ya biashara ndogo ndogo, michezo, masuala ya vijana,biashara na uwekezaji.
Kwa upande wake, waziri wa mambo ya kigeni wa Kenya, Musalia Mudavadi, amesema kwamba ziara ya rais Museveni ni muhimu zaidi na inalenga kuimarisha pakubwa uhusiano kati ya mataifa hayo ya Afrika Mashariki.
I am delighted to be in Kenya today at the invitation of H.E. Ruto. This serves as a platform to further strengthen the strong historical ties between Uganda and Kenya. I look forward to having fruitful discussions during this visit. pic.twitter.com/aFTpPK2Ie0
— Yoweri K Museveni (@KagutaMuseveni) May 15, 2024
Aidha Mudavadi ameeleza kwamba ziara hiyo pia inalenga kufanya tathmini ya hatua zilizopigwa katika makubaliano ya awali kati ya nchi hizo jirani.
Masuala ibuka katika nchi za ukanda na kimataifa pia yatajadiliwa wakati wa kikao cha wakuu hao kutoka Kenya na Uganda.