Pata taarifa kuu

Kenya: Watu wawili wamefariki katika mlipuko wa gesi, 222 wajeruhiwa

Nairobi – Karibia watu wawili wamethibitishwa kufariki katika mtaa wa Embakasi jijini Nairobi nchini Kenya, wakati wengine karibia 222 wakiendelea kupokea matibabu baada ya kutokea mlipuko mkubwa wa gesi usiku wa kuamkia leo.

Kwa sasa serikali inaendelea na uchunguzi kubaini chanzo halisi cha mlipuko huo
Kwa sasa serikali inaendelea na uchunguzi kubaini chanzo halisi cha mlipuko huo REUTERS - THOMAS MUKOYA
Matangazo ya kibiashara

Picha zilizonaswa kwenye eneo la tukio zimeonyesha nyumba, biashara na magari yakiwa yameharibiwa vibaya moto mkubwa ukiwaka karibu na majengo ya ghorofa.

Inadaiwa kuwa huenda moto huo ulisababishwa na mlipuko uliotokea kwenye lori la kusafirisha mitungi ya gesi licha ya hapo awali msemaji wa serikali ya Kenya kudai kuwa  mlipuko huo ulitokea katika kiwanda cha gesi.

Licha ya taarifa hizo za kukinazana kuhusu chanzo cha mlipuko huo, mashahidi wanadai kuwa chanzo kilikuwa ni kiwanda kinachodaiwa kujishugulisha na biashara ya mitungi ya gesi.

Hapo awali, shirika la msalaba mwekundu la Kenya lilikuwa limeripoti karibu watu 300 waliojeruhiwa.

Moto huo ulizuka Alhamisi usiku katika kitongoji cha Embakasi kusini mashariki mwa mji mkuu.Wakaazi wengi wa eneo hilo walilala nje usiku kucha.

Polisi wamezingira eneo lililoathiriwa, lakini baadhi ya watu walionekana wakikusanya mali zao na kuchunguza uharibifu huo.

Vyombo vya habari vya ndani vimeripoti kuwa baadhi ya wakazi kwenye eneo hilo wameanza kuondoka kwa hofu ya kutokea mlipuko mwengine
Vyombo vya habari vya ndani vimeripoti kuwa baadhi ya wakazi kwenye eneo hilo wameanza kuondoka kwa hofu ya kutokea mlipuko mwengine REUTERS - THOMAS MUKOYA

Mnamo 2018, moto katika soko la Gikomba jijini Nairobi uliua watu 15 na kujeruhi takriban 70.

Mamlaka kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki kwa sasa inaendelea kuchunguza kubaini chanzo halisi cha mlipuko huo wa usiku wa kuamkia leo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.