Fahali aliyemuua mchungaji wake auawa Mgaharibi ya Kenya
Nairobi – Nchini Kenya, fahali anayemilikiwa na seneta wa jimbo la Kakamega Magharibi ya taifa hilo la Afrika Mashariki, hapo jana Jumapili amemuua mchungaji wake.
Imechapishwa:
Kwa mujibu wa Seneta Boni Khalwale, mmiliki wa fahali huyo maarufu kama Inasio, aliripotiwa kumuua Kizito Moi, ambaye amekuwa akimtunza pamoja na fahali wengine kwa kipindi cha zaidi ya miaka 20.
Mwili wa mchungaji huyo ulipatikana ukiwa na majeraha makubwa kichwani, shingoni, tumboni na mgongoni asubuhi ya Jumapili iliopita.
Tragedy as fighter bull kills Senator Khalwale's caretaker pic.twitter.com/l9QEYn5CEj
— Citizen TV Kenya (@citizentvkenya) January 28, 2024
Kulingana na tamaduni za kabila la waluyha anakotokea Seneta huyo, fahali huyo aliuawa na kisha nyama yake kugawanywa baina ya wanakijiji.
Fahali huyo mwenye umri wa miaka mitano, aliyekuwa na uzani wa kilo 120, alikuwa ametawazwa hivi majuzi kuwa bingwa wa mashindano ya kupiganisha mafahali, mchezo maarufu Magharibi ya Kenya.
My champion bull, Inasio, has attacked and instantly killed Kizito Moi Amukune. Moi has been the caretaker of my fighter bulls for over 20 years.
— Dr Boni Khalwale, CBS (@KBonimtetezi) January 28, 2024
In keeping with our culture, I have today speared bull Inasio to death. pic.twitter.com/mQszm6ZzOW
Seneta ni miongoni mwa watu maarufu ambao wamekuwa wakiandaa mashindano ya kuwapiganaisha mafahali, shughuli ya kitamaduni inayoenziwa na wengi haswa katika kaunti ya Kakamega.
The late Inasio became champion on 1/01/2024.. pic.twitter.com/HQsrJtEj4M
— Dr Boni Khalwale, CBS (@KBonimtetezi) January 28, 2024