Pata taarifa kuu

DR Congo: Serikali kufuatilia kesi dhidi ya mwanahabari Stanis Bujakera

Nairobi – Serikali ya DRC, kupitia waziri wake wa mawasiliano, Patrick Muyaya, imesema inafuatailia kwa karibu kesi dhidi ya mwanahabari Stanis Bujakera, aliyakamatwa kwa tuhuma za kuandika habari za uongo kuhusu kifo cha waziri wa zamani Cherubin Okende.

Mwanahabari huyo ametakiwa na idara ya ujasusi kuweka wazi vyanzo vya taarifa yake
Mwanahabari huyo ametakiwa na idara ya ujasusi kuweka wazi vyanzo vya taarifa yake © Avec l'aimable autorisation de actualite.cd
Matangazo ya kibiashara

Stanis Bujakera anadaiwa kusambaza taarifa za uongo kuhusu ripoti iliyo chapiswa na Jeune Afrique ikihusisha ujasusi wa kijeshi katika mauaji ya aliyekuwa waziri wa zamani Chérubin Okende.

Baada ya  kukamatwa kwake katika uwanja wa ndege wa Ndjili wakati akitarajia kwenda mjini Lubumbashi, simu zake na kompyuta zilichukuliwa na vyombo vya usalama.  

Aliyekuwa waziri wa zamani Chérubin Okende
Aliyekuwa waziri wa zamani Chérubin Okende AP - Samy Ntumba Shambuyi

Mwanahabari huyo ametakiwa na idara ya ujasusi kuweka wazi waliompa taarifa hiyo.

Waandishi wa habari nchini DRC wanasema wameghadhabidshwa na kukamatwa kwa mwenzao. Kwa mujibu wa  EDMOND IZUBA, msemaji wa muungano wa waandishi wa habari wa Kongo amesema, taarifa iliyochapishwa na Jeune Afrique haina saini yake.

Ikiwa serikali iliona ripoti hio ambayo ilichapiswa na jeune Afrique ni ya uongo, basi wangefuata kipengele cha 104 kuhusu sheria ya uhuru wa vyombo vya habari inayowapa nafasi watupilie mbali tuhuma ya ripoti hio.”alieleza Edmond Izuba.

00:18

Edmond Izuba- Msemaji wa Muungano wa wanahabari nchini DRC

Shirika la kutetea haki za binadamu la voix des sans voix limeomba vyombo vya sheria kutoa mwanga kuhusu mauaji ya waziri huyo wa zamani ambaye pia alikuwa mtu wa karibu wa mwanasiasa wa upinzani MOISE KATUMBI.

Moïse Katumbi, amepata uungwaji mkono wa waziri mkuu wa zamani Matata Ponyo
Moïse Katumbi, amepata uungwaji mkono wa waziri mkuu wa zamani Matata Ponyo © RFI/France24

Ronsard MANKETA ni katibu mtendaji wa shirika hilo.

Ingekuwa vizuri aachiliwe huru kuliko kupelekwa katika gereza la Makala, mahakama ya Kongo inatakiwa kuleta mwanga kuhusu mauaji ya mbunge Chérubin Okende, kuliko kumshambulia mwandishi wa habari ambaye alifanya kazi yake.” alisema Ronsard Manketa.

00:10

Ronsard Manketa

Kwa upande wake waziri wa habari aliahidi kufuatilia kwa karibu suala hili. “Hili ni swali ambalo liko chini ya mamlaka ya mahakama” alisema Patrick Muyaya.

Balozi kadhaa zimeelezea wasiwasi wao kuhusu hali ya mwanahabari huyo wakati huu ikiwa imesalia miezi mitatu kabla ya uchaguzi mkuu unaopangwa kufanyika tarehe 20 Desemba.

Freddy Tendilonge/ Kinshasa/RFI Kiswahili

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.