Pata taarifa kuu

Kenya: Rais Ruto atoa wito wa kushtakiwa kwa mhubiri mwenye imani potofu

NAIROBI – Rais wa Kenya William Ruto ametoa wito wa  kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa Paul Mackenzie mchungaji wa kanisa anayekabiliwa na utata baada ya wafuasi wake zaidi ya 40 kufariki wakisusia kula.

 William Ruto, Rais wa Kenya
William Ruto, Rais wa Kenya REUTERS - MONICAH MWANGI
Matangazo ya kibiashara

Mackenzie anadaiwa kuwaagiza wafuasi wake wa kanisa la Good News International pwani ya Kenya, kutokula chakula hadi wafariki akiwahidi kuwa hiyo ingekuwa njia rahisi ya kukutana na Yesu Kristo kwa haraka.

Rais Ruto katika taarifa yake amemtaja mchungaji  huyo kama mtu gaidi anayestahili kuchukuliwa hatua za kisheria.

Wito wa rais Ruto unakuja wakati huu ambapo pia, raia na mashirika ya kutetea haki za binadamu katika taifa hilo la Afrika Mashariki wakiishinika serikali kumchukulia hatua kali mchungaji huyo kutokana na imani yake ya kupotosha raia.

Mhubiri anaekabiliwa na utata nchini Kenya
Mhubiri anaekabiliwa na utata nchini Kenya © kbc

Kauli ya mkuu wa nchi ikija muda mfupi baada ya Polisi kupata mwili mitatu zaidi kutoka kwenye kaburi la pamoja karibu na mji wa pwani wa Malindi. Hii inafikisha idadi ya waliofariki kufika watu 42.

Maafisa wakuu wa usalama wakiongozwa na Inspekta Jenerali wa Polisi, Japhet Koome na mkurugenzi mkuu wa idara  ya Upelelezi wa makosa ya Jinai Mohamed Amin wakitarajiwa kujiunga na kikosi cha wachunguzi katika eneo Shahola palipopatikana makaburi hayo.

Wafuasi wa mchungaji wa mchungaji  Paul Mackenzie waliaamini kuwa iwapo wangefariki kutokana na njaa basi wangekutana na kristo kwa haraka.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.