Pata taarifa kuu

DRC: Wakimbizi waandamana Goma wakitaka chakula

NAIROBI – Polisi jijini Goma wamewatawanya raia hao walioandamana wakilalamikia mateso wanayoyapitia kambini bila ya  kupata msaada. Raia huyu wa Goma ni miongoni mwa walioandamana

Wakimbizi katika kambi ya Kanyaruchinya mjini Goma wameandamana wakiituhumu serikali ya DRC kwa ukosefu wa chakula katika kambi hiyo.
Wakimbizi katika kambi ya Kanyaruchinya mjini Goma wameandamana wakiituhumu serikali ya DRC kwa ukosefu wa chakula katika kambi hiyo. AFP - GLODY MURHABAZI
Matangazo ya kibiashara
00:17

Raia wa Goma

“Watoto wana njaa na Sisi hatuna hata pesa ya kununua chakula, ombi letu nikupata haki yetu ya kupata chakula kama sivyo waturejeshe kwetu ambako kuna waasi wa M23.”amesema raia wa Goma.

Watetezi wa haki za binadamu pamoja na baadhi ya raia hao walioandamana wamesema kutokana na changamoto wanazozipitia zimesababisha baadhi yao kuamua kurejea katika vijiji vyao vya kawaida wilayani Masisi na Rutshuru, licha ya ukosefu wa usalama vijijini mwao.

Bose Bamwe jean Étienne ni mtetezi wa haki za binadamu kutoka shirika la Acadepa wilayani nyiragongo.

00:15

Bose Bamwe jean Étienne ni mtetezi wa haki za binadamu Goma

“Imepita sasa  zaidi ya miezi miwili bila kupata msaada wa chakula,tunataka serikali yetu na wahusika wa masuala ya kijamii kusaidia watu hawa walio hatarini.”amesemaBose Bamwe jean Étienne ni mtetezi wa haki za binadamu kutoka shirika la Acadepa wilayani nyiragongo.

Nzangi Butondo ni waziri anayehusika na masuala ya elimu na vyuo vikuu nchini Congo DR.

00:10

Nzangi Butondo

“inabidi serikali ipange vizuri huduma ya kugawa misaada ilipasitokee tena shida.”amesema Nzangi Butondo

Haya yanajiri wakati huu waasi wa M23 wakiendelea kushutumiwa kwa kutekeleza mashambulio dhidi ya raia wa eneo la mashariki.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.