Pata taarifa kuu

DRC: Wanaharakati wana mashaka na ahadi za M23 kuondoka Rumangabo

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, waasi wa M 23 wanatarajiwa kuondoka na kukabidhi Rumangabo, kambi kubwa ya wanajeshi wa DRC kwa vikosi vya Jumuiya ya Afrika Mashariki, baada ya kuahidi kuondoka. 

Waasi wa M23 katika eneo la Rumangabo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Julai 28, 2012.
Waasi wa M23 katika eneo la Rumangabo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Julai 28, 2012. REUTERS/James Akena
Matangazo ya kibiashara

Waharakati wanasema hawaamini iwapo waasi hao wataondoka kabisa katika eneo hilo la  kambi ya Rumangambo, baada ya kuondoka kwao mjini Kibumba kutiliwa shaka na jeshi la DRC, kama anavyoeleza HENRI MAHANO, kiongozi wa Shirika la kirai katika eneo hilo. 

Wakati hili likitarajiwa, ripoti zinasema jana; waasi hao waliendelea kusonga mbele katika Wilaya ya Rutshuru na kuchukua eneo la Nyamilima. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.