Pata taarifa kuu
JAMUHURI YA KIDEMOKRASIA YA CONGO-ICC

Kesi ya afisa wa zamani wa jeshi nchini DRC Bosco Ntaganda inasikilizwa mjini The Hague

Mahakama ya uhalifu ya kivita ya ICC inataraji kusikiliza leo Jumatatu kesi ya mauaji ya kivita inayo mkabili mbabe wa zamani wa kivita nchini DRCongo Bosco Ntaganda aliye julikana kama Terminator kufuatia ukatili wake.

Bosco Ntaganda, afisa wa zamani wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, akiwa mahakamani The Hague, ICC
Bosco Ntaganda, afisa wa zamani wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, akiwa mahakamani The Hague, ICC RFI
Matangazo ya kibiashara

Mahakama hiyo itaamuwa iwapo tuhuma za ubakaji, mauaji na uporaji vilivyotekelezwa mashariki mwa DRCongo. Wananchi wa maeneo hayo wanasubiri kwa hamu na gamu kesi.

Kiongozi wa zamani waasi nchini Congo (DRC) Bosco Ntaganda alijisalimisha machi 17 mwaka 2013 katika ubalozi wa marekani  nchini Rwanda ambako alikimbilia.

Bosco alikuwa akitafutwa na mahakama ya uhalifu wa kivita ICC.

Kwa mara ya kwanza akipandishwa kizimbani kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ya ICC, jenerali Bosco Ntaganda alisisitiza kuwa hana hatia kuhusu tuhuma zinazomkabili mbele ya mahakama hiyo.

Jenerali Ntaganda anakabiliwa na mashtaka kumi ikiwemo kuamuru Ubakaji, mauaji na kutumia watoto kwenye jeshi lake kufanya uasi mashariki mwa nchi hiyo.

Ntaganda aliyekuwa akifahamika kama "The Terminator" alishirikiana na makundi mengi ya uasi mashariki mwa nchi hiyo licha ya kuwa aliwahi kuwa kiongozi wa juu kwenye jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.