Pata taarifa kuu
SUDANI KUSINI-Umoja wa mataifa

Kikosi cha kwanza cha kulinda amani Sudan kusini chawasili

Kikosi cha kwanza cha umoja wa mataifa UN cha kulinda amani huko sudan kusini kimewasili jana ijumaa nchini humo wakati huu umoja wa mataifa ukionya hali ya mvutano kuendelea kuhatarisha usalama licha ya jitihada za kuandaa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya serikali na majeshi ya uasi.

kikosi cha umoja wa Mataifa UN kimewasili kulinda amani  Sudan Kusini
kikosi cha umoja wa Mataifa UN kimewasili kulinda amani Sudan Kusini RFI
Matangazo ya kibiashara

Kikosi hicho kikitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kilikuwa cha kwanza kikiwa na askari takribani elfu 6 walioidhinishwa na Baraza la Usalama kuimarisha usalama huko sudan kusini.

Umoja wa Mataifa ulitahadharisha hatari iliyopo huku bado idadi kubwa ya miili ambayo haikuweza kukusanywa imeonekana katika kambi za umoja wa mataifa.

Hapo jana duru ziliarifu kuwa Waasi wanaomuunga mkono aliyekuwa Makamu wa rais wa Sudan Kusini Salva Kiir wanajiandaa kukabaliana na vikosi vya serikali katika jimbo la Unity lenya utajiri wa Mafuta.

Haya yanafanyika kipindi hiki viongozi wa nchi wanacaham wa IGAD wakikutana jijini Nairobi nchini Kenya kujaribu kupata suluhu kuhusu hali ya usalama na kisiasa nchini Sudan Kusini.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.