Pata taarifa kuu
MALI

Ansar Dine wataka makundi mengine kuunga mkono juhudi za amani Mali

Kundi la Ansar Dine linaloshikilia sehemu ya eneo la Kaskazini mwa Mali lililoangukia kwenye mikono ya Makundi ya wailsam wenye msimamo mkali limetoa wito kwa makundi mengine kushiriki kwenye mazungumzo ya kisiasa. 

Wajumbe wa kundi la Ansar Dine katika mazungumzo ya amani nchini Mali
Wajumbe wa kundi la Ansar Dine katika mazungumzo ya amani nchini Mali au.news.yahoo.com
Matangazo ya kibiashara

Mwakilishi wa Kundi la Ansar Dine Mohamed Aharid ambaye amekutana na msuluhishi wa mgogogoro huo ambaye ni rais wa Burkina Faso Blaise Compaore ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha hali ya kisiasa inarejea kama awali.

Katika tamko lililosomwa na mjumbe huyo, kundi hilo limetoa tamko la kusitisha uhasama, kuheshimu haki za msingi na uhuru wa binadamu, kuwarejesha watu wote waliokimbia makazi yao na wakimbizi na kutengeneza mazingira rafiki kwa ajili ya kutekeleza kikamilifu makubaliano ya amani ambayo ni chanzo kikuu cha mgogoro.

Kauli ya Ansar Dine inakuja kipindi hiki ambacho Wataalam wa Masuala ya Kijeshi kutoka Afrika, Marekani na Ulaya wakipanga mbinu za kupeleka Jeshi lao na hapa Ngari Gituku anaangalia kile kinachoendelea katika Taifa hilo.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.