Pata taarifa kuu
MAREKANI

Chama cha Republican chamuidhinidha rasmi Mitt Romney kupeperusha bendera katika mbio za uraisi

Chama cha Republican nchini Marekani kimemuidhinisha rasmi Mitt Romney kupeperusha bendera ya chama hicho katika mbio za uraisi wa nchi hiyo unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu ambapo atamkabili raisi wa sasa Barack Obama.

Mgombea wa uraisi kwa tiketi ya Republican Mitt Romney akiwa na mkewe Anna Tampa,katika mkutano wa chama cha Republican.
Mgombea wa uraisi kwa tiketi ya Republican Mitt Romney akiwa na mkewe Anna Tampa,katika mkutano wa chama cha Republican. REUTERS/Jason Reed
Matangazo ya kibiashara

 

Romney sambamba na mkewe walijumuika na wanachama wengine wa Republican ambao walijitokeza kwa wingi jimboni Florida kutoa shukurani zake kwa chama cha Republic.

Mitt Romney anatarajiwa kutoa changamoto kwa mpinzani wake kutoka chama cha Democratic raisi wa sasa wa taifa hilo Barack Obama katika uchaguzi mkuu wa raisi mnamo mwezi Novemba ambapo changamoto mbalimbali bado zimeelezwa kuikabili Marekani ikiwemo kuyumba kwa uchumi na tatizo la ajira.

Kabla ya kuidhinishwa kuwa mgombea rasmi wa Chama Cha Republican kwenye mkutano mkuu wa Chama hicho Romney alipaswa kuungwa mkono na wajumbe elfu moja mia moja na arobaini na nne ndiyo kupata ridhaa ya kuwa mgombea.

Nafasi ya Romney ilizidi kuwa kubwa baada ya baadhi ya wagombea kujiondoa kwenye mbio za kusaka kuteuliwa kuwa mgombea kupitia tiketi ya Chama Cha Republican kwenye uchaguzi wa baadaye mwaka huu.

Mkutano wa chama cha Republican ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu ili kumbaini mgombea ambaye atapeperusha bendera ya chama hicho.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.