Pata taarifa kuu
BAHRAIN

Muandamanaji wa kishia auwawa na polisi nchini Bahrain

Polisi nchini Bahrain wamemuua muandamanaji mmoja wa kishia baada ya kurusha mabomu ya machozi kujaribu kuwatawanya waandamanaji wapinzani nchini humo wameeleza

Baadhi waandamanaji nchini Bahrain.
Baadhi waandamanaji nchini Bahrain. Reuters
Matangazo ya kibiashara

Taarifa zaidi kutoka kundi la upinzani la washia zinasema kuwa muandamanaji huyo Sayyed Hashem Saeed,mwenye umri wa miaka 15, alipigwa na bomu kichwani na mtu aliyejaribu kumsaidia alijeruhiwa eneo la paja.

Wakati huohuo mkuu mpya wa polisi aliyeteuliwa hivi karibuni amesema kuwa askari wapatao mia tano watasambazwa nchi nzima ikiwa ni pamoja na washia kusaidia kukuza mahusiano ya jamii wakati nchi inajaribu kujifunza kutokana na machafuko yaliyopita.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.