MISRI
UNICEF yaagiza watoto walindwe nchini Misri.
Kufuatia kuendelea kwa machafuko nchini Misri kati ya waandamanaji na polisi na kushuhudia watu kadhaa wakipoteza maisha wakiwemo watoto, shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia watoto duniani UNICEF limeitaka serikali ya kijeshi nchini humo kuwalinda watoto.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kwa mujibu wa taarifa ya shirika hilo imesema kuwa watoto wawili wameuawa toka kuanza kwa machafuko ya hivi karibuni huku wengine zaidi ya 70 wakielezwa kushikiliwa kwenye magereza mbalimbali nchini humo.