Pata taarifa kuu
SRI LANKA

Mataifa makubwa yasusia mafunzo ya Sri Lanka ya kukabiliana na ugaidi

Mataifa matano yenye nguvu duniani, yamesusia semina ya namna ya kupambana na ugaidi iliyoandaliwa na serikali ya Sri Lanka kwa madia kuwa, nchi hiyo ilihusika katika mauaji ya raia wakati wa oparesheni ya kulitokomeza kundi la Tamil Tigers.

Viongozi wa serikali ya Sri Lanka wakijadili juu ya kukabiliana na waasi wa Tamil Tigers
Viongozi wa serikali ya Sri Lanka wakijadili juu ya kukabiliana na waasi wa Tamil Tigers AFP/Ishara S. Kodikara
Matangazo ya kibiashara

Miongoni mwa mataifa yaliyokataa kushiriki katika semina hiyo ni pamoja na Marekani, Uingereza, Ufaransa na Ujapan ambazo zote kwa pamoja zimeitaka serikali ya nchi hiyo kuchunguza kwa kina mauaji ya raia.

Taarifa kutoka katika waandaaji hao, inapasha kuwa serikali ya Sri Lanka, ilifanikiwa kuwashinda waasi hao, kutokana na kujifunza kwa miaka mingi jinsi ya kupambana na wavamizi, sanjari na utayari thabiti wa kisiasa pamoja na kuungwa mkono.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.