Pata taarifa kuu
SIASA-HAKI

Nicaragua yawaachilia zaidi ya wafungwa 200 wa kisiasa wakiwemo wanawake wawili wa Ufaransa

Zaidi ya wafungwa 200 wa upinzani, wakiwemo wanawake wawili wa Ufaransa, wameachiliwa Alhamisi, Februari 9 huko Nicaragua na serikali ya Daniel Ortega na wako njiani kuelekea Marekani, ndugu na wapinzani walio uhamishoni wamesema.

Picha iliyotolewa na ikulu ya rais wa Nicaragua inaonyesha Dora María Téllez akiwasili chini ya ulinzi wa polisi katika mahakama kwa ajili ya kusikilizwa huko Managua, Agosti 31, 2022.
Picha iliyotolewa na ikulu ya rais wa Nicaragua inaonyesha Dora María Téllez akiwasili chini ya ulinzi wa polisi katika mahakama kwa ajili ya kusikilizwa huko Managua, Agosti 31, 2022. AFP - CESAR PEREZ
Matangazo ya kibiashara

"Wafungwa 222 wa kisiasa wanawasili Washington, wameachiliwa huru," amesema katika video iliyotumwa kwenye mitandao ya kijamii Arturo McFields, balozi wa zamani wa Nicaragua katika Umoja wa Mataifa ya Amerika (OAS), ambaye aliondolewa madarakani baada ya kuita nchi yake ya udikteta na ambaye sasa anaishi Marekani.

Javier Alvarez, raia wa Nicaragua anayeishi uhamishoni nchini Costa Rica, amelithibitishia shirika la habari la AFP kwamba miongoni mwa walioachiliwa ni mke na binti yake, ambao pia wana uraia wa Ufaransa. Managua bado hajatoa taarifa yoyote rasmi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.