Covid 19: Zaidi ya kesi mpya 240,000 na vifo 3,000 vyathibitishwa nchini Marekani
Vituo vya Marekani vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) Jumamosi vimeripoti visa 244,011 zaidi kuliko siku moja kabla na vifo vipya 3,013, na kusababisha idadi ya fifo kufikia 294,535 kwa jumla ya visa 15,718,811 vya maambukizi .
Imechapishwa:
Siku ya Ijumaa rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kuwa chanjo ya kwanza ya COVID-19 nchini Marekani itaanza kutolewa hivi punde.
Mamlaka ya kukagua Chakula na Dawa Marekani, FDA, ilitoa idhini ya matumizi ya dharura ya chanjo ya COVID-19 iliyotengenezwa na maambara ya Pfizer na BioNTech.
FDA inatarajiwa kuidhinisha leo Jumapili chanjo mpya ya kupambana na virusi vya Corona.
Afisa wa FDA hivi karibuni alisema uamuzi kama huo unaweza kuchukua wiki kadhaa.
Donald Trump, ambaye aliweka shinikizo kwa maabara, anaweza kurekodi ushindi wa mwisho pamoja na uuzaji wa chanjo hiyo wiki chache kabla ya kumkabidhi madaraka mrithi wake Joe Biden.