Mauaji ya Breonna Taylor: Taharuki yatanda Marekani, maafisa 2 wa polisi wajeruhiwa kwa risasi
Maafisa wawili wa Polisi wamepigwa risasi wakati maelfu ya watu wakiandamana katika mji wa Louisville baada ya Mahakama kuamua waliomuua mwanamke mweusi Breonna Taylor hawatachukuliwa hatua.
Imechapishwa:
Hasira za waandamanaji zimesababihwa na Bi Taylor mwenye umri wa miaka 26, kupigwa risasi mara kadhaa baada ya maafisa wa usalama kumvamia nyumbani kwake mwezi Machi.
Kilichochea maandamano hayo ni afisa anayeshukiwa kutekeleza mauji hayo Brett Hankison, amefunguliwa mashataka tofauti, kinyume na matarajio ya wengi , huku maafisa wengine wawili wakisalia huru bila kufunguliwa mashtaka yoyote.
Licha ya kupigwa risasi wakati wa maandamano hayo, ripoti zinasema kuwa hali za maafisa wawili wa polisi sio mbaya sana na wanaendelea kupokea matibabU, huku mshukiwa akimatwa.
Kutoana na vurugu zinazoshuhudiwa, hali ya hatari imetangazwa katika mji wa Louisville na jeshi la akiba kutumwa katika mji huo.
Marekani imeendelea kukumbwa na visa vya mauaji ya watu weusi, vitendo vinavyohusishwa maafisa polisi wazungu, na kuacha maswali mengi kuhusu uwezo wa taifa hilo kupambana na ubaguzi wa rangi.