Uchaguzi Marekani: Donald Trump amtetea mshauri wake
Meneja wa Kampeni za mwasiasa wa chama cha Republocan nchini Marekani Donald Trump, amefunguliwa mashhtaka ya kumvamia na kumjeruhi mwandishi wa Habari wakati wa mkutano wa kisiasa.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Wow, Corey Lewandowski, my campaign manager and a very decent man, was just charged with assaulting a reporter. Look at tapes-nothing there!
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) March 29, 2016
Donald Trump haraka amelaani uamuzi huo na kusema kuwa ana mashaka na uhalali wa malalamiko ya mshitaki wake.
Corey Lewandowski, ambaye aliripoti kwa hiari yake
Because my story never changed. Seriously, just stop lying. https://t.co/1fz9cBHOuT
— Michelle Fields (@MichelleFields) March 29, 2016
mbele ya polisi ya Jupiter katika mji wa Florida, amefahamishwa kuripoti Mei 4 kwa tuhuma za kumvamnia na kumjeruhi mwanahabari Michele Fields, ambaye alijaribu kumhoji Donald Trump baada ya mkutano na waandishi wa habari kuhusu klabu yake ya gofu mjini Florida, Machi 8.
Why is this reporter touching me as I leave news conference? What is in her hand?? pic.twitter.com/HQB8dl0fhn
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) March 29, 2016
Hata hivyo Corey Lewandowski amekanusha tuhuma dhidi yake.
Polisi wanasema wana mkanda wa Video unaothibitisha kuvamiwa kwa mwanahabari huyo.
Meneja huyo anatarajiwa kufikishwa tena Mahakamani hivi karibuni.