Pata taarifa kuu
Venezuela

Rais Hugo Chavez kuteta kiti cha urais mwakani licha ya matatizo ya kiafya

Licha ya matatizo ya kiafya yanayomkabili Rais wa Venezuela Hugo Chavez, msaidizi wake amesema wazi kuwa, kiongozi huyo amepania kutetea nafasi yake, katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika, hapo mwakani.

Hugo Chávez rais wa Venezuela
Hugo Chávez rais wa Venezuela Reuters
Matangazo ya kibiashara

Akihojiwa na luninga ya taifa, waziri wa fedha wa Venezuela Jorge Giordani, ametoa kauli hiyo, wakati Chavez akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa saratani, nchini Cuba.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 56, ameliongoza taifa hilo, kwa miana kumi na miwili, na angependa kuendelea kushika wadhifa huo, kwa miaka mingi zaidi.

Na kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais wa Cuba Fidel Castro, amewafariji raia wa Venezuela na kuwahakikishia kuwa Chavez, anaendelea vema.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.