Marekani
Matumaini ya kuwapata watu waliohai baada ya kufunikwa na kimbunga nchini Marekani yatoweka
Kikosi cha waokoaji na wanafamilia walionusurika kwenye kimbunga nchini Marekani kilichosababisha vifo vya watu zaidi ya mia moja na ishirini na tano wanaendelea kusaka miili ya watu walionaswa kwenye mabaki ya vifusi.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Zoezi hili linaendelea kushika kasi wakati taarifa zinaeleza maiti kumi na tano nyingine zimepatika kwenye msako huo ulioleta madhara makubwa kwenye eneo la Missouri na kuwaacha maelfu bila ya makazi.
Mkuu wa Zimamoto ambaye anaongoza Kikosi Maalum cha Waokoaji Mitch Randles amesema wamekata tamaa ya kupata watu waliohai lakini wataendelea kusaka miili hiyo kwenye malundo ya vifusi.