Pata taarifa kuu

Sudan: Hamdan Daglo anatuhumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita

Nairobi – Kiongozi wa kikosi cha wanamgambo nchini Sudan cha RSF Mohamed Hamdan Daglo anatuhumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita nchini Sudan, wakati huu  akiendeleza ziara yake kwa mataifa ya Kikanda, ziara inayondekana kuwagawa msimamo ya viongozi wa kikanda.

Dagalo ameonekana kupata ungwaji mkono kutoka utawala wa Chad kuhusu kinachoendelea nchini Sudan
Dagalo ameonekana kupata ungwaji mkono kutoka utawala wa Chad kuhusu kinachoendelea nchini Sudan REUTERS - MOHAMED NURELDIN ABDALLAH
Matangazo ya kibiashara

Hamdan Daglo amekua akifanya safari za kikanda ikiwa ni juhudi za kujaribu kujaribu kutafuta ungwaji mkono na viongozi wa kikanda na bara Afrika, kujaribu kusuluhisha mzozo ambao umepelekea vita kati ya kikosi chake cha RSF na jeshi la Sudan.

Kiongozi huyo wa RSF pia alizuru Afrika Kusini ambapo alikutana na rais Cyril Ramaphosa
Kiongozi huyo wa RSF pia alizuru Afrika Kusini ambapo alikutana na rais Cyril Ramaphosa via REUTERS - GOVERNMENT COMMUNICATION AND INF

Hamdan amefanya mazungmzo na marais wa Kenya, Uganda, Afrika Kusini, Rwanda, na Djibouti pamoja na Ethiopia, ili kutafta njia mwafaka ya kumaliza mzozo na kwamba mchakato wa amani unaoendelezwa na IGAD, unastahili kufikia suluhu ya kisiasa itakayoleta amani ya kudumu nchini humo, ambapo kiongozi huyo anapata ungwaji mkono kutoka utawala wa Chad.

Naye kiongozi wa utawala wa kijeshi nchini Sudan Abdel Fattah Al-Burhan akionekana kupata ungwaji mkono kutoka kwa Misri na Eritrea.

Utawala wa Jenerali Abdel Fattah al-Burhan,umekuwa ukipambana na kundi na RSF nchini Sudan
Utawala wa Jenerali Abdel Fattah al-Burhan,umekuwa ukipambana na kundi na RSF nchini Sudan © AFP PHOTO / HO/ SAUDI PRESS AGENCY

Hivi majuzi wapiganaji wa RSF nchini Sudan wameonesha utayari wao wa kusitisha mara moja mapigano na bila masharti yoyote kupitia mchakato wa mazungumzo na Jeshi la Sudan.

Vita  nchini Sudan vilivyoanza mwezi Aprili mwaka jana, na tayari vimesababisha vifo vya zaidi ya watu 12,000 huku Umoja wa Mataifa ukisema kuwa zaidi ya watu milioni 7 wameyakimbia makazi yao.

Mkuu wa RSF nchini Sudan Mohamed Hamdan Dagalo alikutana na rais wa Kenya, William Ruto
Mkuu wa RSF nchini Sudan Mohamed Hamdan Dagalo alikutana na rais wa Kenya, William Ruto © William Ruto

Tume ya umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS, hapo jana ililaani vurugu zilizosababisha vifo vya raia 28 kwenye mji wa Duk, kaunti ya Jonglei.

UNMISS sasa inawataka viongozi wa eneo la Jonglei na Pibor, kukutana kwa mazungumzo ili kuepuka mashambulio ya ulipizaji kisasi baada ya vijana wa Murle kutekeleza mauaji hayo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.