Pata taarifa kuu

Sudan: Marekani yatoa wito kwa RSF kuacha kushambulia maeneo ya raia

Marekani imewataka wapiganaji wa RSF nchini Sudan kuacha kushambulia kwa makombora maeneo ya makazi ya raia, Washington ikisema hatua hiyo inazidisha mateso kwa raia Sudan.

Mazungumzo ya amani yaliyoongozwa na Marekani na Saudi Arabia kati ya RSF na jeshi yalivunjika mwezi Julai
Mazungumzo ya amani yaliyoongozwa na Marekani na Saudi Arabia kati ya RSF na jeshi yalivunjika mwezi Julai REUTERS - MOHAMED NURELDIN ABDALLAH
Matangazo ya kibiashara

Kupitia taarifa, wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani imetoa wito kwa RSF kuhakikisha raia katika maeneo ya Nyala, Omdurman, na kote Sudan wanalindwa badala ya kuwashambulia.

Wapiganaji wa  RSF na jeshi la Sudan wamekuwa wakipigana tangu Aprili katika mzozo ambao umesababisha vifo vya zaidi ya watu 5,000 na wengine zaidi ya milioni tano kukimbia makazi yao, kulingana na ripoti ya UN.

Katika siku za hivi majuzi RSF imeonekana kuongeza  mashambulio kwenye maeneo yanayodhibitiwa na jeshi huko Omdurman, hatua ambayo imesababisha vifo vya raia.

Sehemu kubwa ya raia wa Sudan wanakabiliwa na uhaba wa chakula na dawa wakati huu mapigano yakiendelea
Sehemu kubwa ya raia wa Sudan wanakabiliwa na uhaba wa chakula na dawa wakati huu mapigano yakiendelea © REUTERS - JOK SOLOMUN

Kundi hilo pia limeendelea kuzingira kambi za kijeshi huko Nyala magharibi mwa jimbo la Darfur kwa nia ya kuuteka mji huo.

Marekani pia imerejelea wito wake kwa RSF na jeshi la Sudan kusitisha mapigano mara moja na kuanza tena mazungumzo ya kumaliza mzozo huo.

Washington tayari imeweka vikwazo kwa makampuni yanayohusishwa na RSF na jeshi, pamoja na viongozi wawili wa RSF wanaotuhumiwa kwa ukiukaji wa haki za binadamu.

Mkuu wa Jeshi la Sudan Jenerali Burhan na kiongozi wa RSF Jenerali  Hemedti wamekuwa wakikabiliana kuhusu suala la uongozi
Mkuu wa Jeshi la Sudan Jenerali Burhan na kiongozi wa RSF Jenerali Hemedti wamekuwa wakikabiliana kuhusu suala la uongozi

Mazungumzo ya amani yaliyoongozwa na Marekani na Saudi Arabia kati ya RSF na jeshi yalivunjika mwezi Julai.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.