Pata taarifa kuu

Libya:Kimbunga Daniel chaua watu zaidi ya 2,000

Nairobi – Takriban watu 2,000 wafariki katika mafuriko yaliyotokea mashariki mwa Libya kutokana na dhoruba ya kimbunga Daniel ambacho kimepiga katika bahari ya Mediterania.

Kimbunga Daniel chapiga libya na kusababisha vifo vya watu 2,000
Kimbunga Daniel chapiga libya na kusababisha vifo vya watu 2,000 AP
Matangazo ya kibiashara

Taarifa hiyo ya vifo vya watu 2,000 imetolewa na Waziri Mkuu wa serikali ya Mashariki mwa Libya Ossama Hamad alipokuwa akihojiwa na kituo cha televisheni cha al-Masar. Vilevile Hamad amasema kuwa kuna idadi kubwa ya raia hawajulikani waliko.

Picha zilizochukuliwa na wakazi wa eneo la maafa, zimeonyesha maporomoko makubwa ya matope, majengo yaliyoanguka na vitongoji vyote vilivyozama chini ya maji.

Shirika la habari la Reuters limeripoti kuwa, picha zilizoonekana kwenye mitandao ya kijamii zilionyesha watu wakiwa wamekwama juu ya magari yao wakati wakijaribu kupata msaada katika mafuriko hayo makubwa, wakati kimbunga Daniel kikipiga miji ya Benghazi, Sousse, Al Bayda, Al-Marj na Derna.

Vikosi vya uokoaji vimepelekwa kwenye mji huo, ulioko takriban kilometa 900 mashariki mwa mji mkuu, Tripoli wakatiu huu Mamlaka zilkitangaza hali ya mbaya ya hatari, na kufunga shule na maduka pamoja na kuweka amri ya kutotoka nje.

Tayari serikali ya Mashariki imetangaza siku tatu za maombolezo kufuatia mkasa huo, Tawfik al Shukri ni msemaji wa shirika la msaada la  Red Crescent.

Wafanyakzi wote  wamekuwepo kila mahali  tangu kutokea kwa mkasa, Jijini Darna, kwa mujibu wa serikali. Kuna zaidi ya miili 2,030 iliyopatikana na zaidi ya watu 9,800 hawajulikani walipo.Kuna vijiji 5 huko Darna ambavyo vimeharibiwa kabisa na maji. Hali ni mbaya sana ... baada ya masaa ya kwanza ya mafuriko, mabwawa yalitolewa. Shirika la  hili  tayari limepoteza wanachama watatu wakati wa oparesheni  ya uokoaji. Lazima tuunganishe juhudi za zetu : serikali mbili za Libya, masharika ya ndani na ya kimataifa ili tuweze kuwasaidia watu kwa uwepesi. Amesema Tawfik al Shukri.

00:35

TAWFIK AL SHUKRI MSEMAJI WA SHIRIKA LA MSAADA LA RED CRESCENT Red

siku za hivi karibuni kimbunga Daniel kilipiga mataifa ya Ugiriki, Uturuki na Bulgaria na kuua watu wasiopungua 27 kutokana na mvua kubwa zilizonyesha.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.